YOUR FUTURE IS CREATED BY WHAT YOU DO TODAY, NEVER TOMORROW

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Ngusa Samike

Mkoa wa Lindi umepokea fedha kiasi cha shilingi Milioni 110 kwa ajili ya ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa Mkoani Lindi

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Ngusa Samike akiwa katika kikao kazi cha uboreshaji wa usimamizi wa Elimu Msingi na Sekondari Mkoani humo kilichofanyika Nyangao Januari 14,2023 amesema kiasi hicho cha fedha ni sehemu ya mgao wa fedha za sherehe za uhuru za mwaka 2022 ambazo zilielekezwa zijenge miundombinu ya watoto wenye mahitaji maalum.

Sambamba na hayo, akizungumzia kuhusu uandikishaji wa wanafunzi wa madarasa ya awali na darasa la kwanza kwa mwaka 2023 amebainisha kuwa hadi sasa Mkoa wa Lindi umeandikisha kwa asilimia 85 ya maoteo.

Naye mkuu wa Wilaya ya Lindi SHAIBU NDEMANGA amewaomba viongozi na wote wanaosimamia sekta ya elimu kusimamia miongozo iliyowekwa kwenye sekta hiyo ili kufikia malengo.

Post a Comment

Previous Post Next Post