Chama
kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA kinatarajia kuzindua ajenda zaidi ya
10 zitakazokiongoza kwenye mikutano yake ya hadhara ambayo inatarajiwa
kuzinduliwa na mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, Januari 21, 2023 jijini Mwanza.
Uzinduzi
wa ajenda hizo utafanyika sambamba na uzinduzi wa mikutano ya hadhara ya chama
hicho kwenye kanda mbili ambazo ni kanda ya Ziwa Viktoria na kanda ya
Serengeti.
Akizungumza
na vyombo vya habari leo Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi na Mambo ya Nje wa
Chadema, John Mrema amesema Mbowe na viongozi wengine wa kitaifa wa Chadema
wataongoza uzinduzi wa mikutano ya hadhara sambamba na ajenda za chama.
Post a Comment