YOUR FUTURE IS CREATED BY WHAT YOU DO TODAY, NEVER TOMORROW
Serikali imeamua kujenga kituo cha kupooza umeme wilayani Kilombero ili kupunguza changamoto ya ukatikaji umeme katika wilaya hiyo.
Mivutano baina ya wataalamu yaani mkandarasi na msimamizi muelekezi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme kitakachoigharimu serikali zaidi ya bilioni 20 kunamfikisha waziri wa nishati Dkt Medard Kalemani wilayani humo mkoani Morogoro na kusikiliza chanzo cha mgogoro unaopelekea ujenzi huo kutoanza kwa wakati na kuagiza ujenzi uanze ndani ya siku kumi kutokana na ujenzi huo kucheleweshwa kwa takribani mwaka mmoja.
Kukamilika kwa kituo hicho kutaondoa changamoto ya kukatika kwa umeme katika wilaya za kilombero,malinyi na ulanga mkoani Morogoro kwani kituo kitakua na uwezo kuingiza na kupooza umeme voltage 220 na kutoa voltage 33 kwa wananchi.
Post a Comment