Polisi, na vyombo vingine vilivyokabidhiwa jukumu la kuhakikisha usalama wa watu na mali zao, hawawezi kukwepa kuhojiwa kuhusiana na wimbi la visa vya utekaji linaloendelea kushamiri nchini hivi sasa, na kuwajaza Watanzania kwa mamilioni hofu juu ya usalama wao na ule wa wanaowapenda.


Kama nchi ambayo wananchi wake wamejiwekea taratibu za kuendesha maisha yao, kama vile kwa kuwa na Katiba inayofanya kazi kama mkataba kati ya wanaoongoza na wanaoongozwa, na kuwa na sera, sheria, kanuni na miongozo zinazofafanua namna mkataba huo unavyopaswa kufanya kazi, ni lazima tuwe na mtu wa kumlaumu pale tunapohisi mambo hayaendi kama wananchi tunavyotarajia.

Wajibu wa kuhakikisha Watanzania wako salama na wanaishi kwa uhuru na amani nchini kwao, bila ya kuwa na hofu ya kupotezwa au kudhuriwa, umekabidhiwa kwa Jeshi la Polisi, na ni wananchi wanaofadhili shughuli zote za taasisi hiyo ili iweze kutimiza wajibu wake huo ipasavyo, ikiwemo kugharamia mishahara ya maafisa wake na stahiki zao zingine.


Cc: Chanzo

Post a Comment

Previous Post Next Post