Kutokana na umuhimu wa Mazoezi ya
mwili kwa binadamu ikiwemo kusaidia katika kudhibiti Magonjwa Yasiyoambukiza ikiwemo kiwango cha
sukari mwilini, pamoja na kupunguza uzito wa mwili, jamii
imeaswa kujenga mazoea ya ya kufanya mazoezi mara kwa mara.
Na. Elimu ya Afya kwa Umma
Hayo yamejiri Jijini
Dodoma katika Utekelezaji wa Mpango wa
Mazoezi na Afya ya Mwili kwa watumishi ndani ya Idara ya Kinga ambapo watumishi
wa idara hiyo wamekuwa na mpango wa kufanya mazoezi kila Jumatatu katika Uwanja
wa Jamhuri Dodoma na kila Jumatano na
Ijumaa katika uwanja wa Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Milembe
Mkurugenzi
Msaidizi Sehemu ya Afya Mazingira , Wizara ya Afya Dkt.Khalid Massa amesema
mazoezi hayo yana umuhimu mkubwa katika kuimarisha Kinga dhidi ya Magonjwa
Yasiyoambukiza.
“Tukiwa katika Wiki hii ya Kudhibiti Magonjwa
Yasiyoambukiza iliyoanza Novemba 11 hadi
18, 2023 tumeendelea na mazoezi hivyo ni vyema viongozi na watu wote
tukaendelea kujumuika na mazoezi haya ni fiti yana umuhimu kuzuia magonjwa yasiyoambukiza”
amesema Dkt.Khalid Massa Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya
Afya Mazingira, Wizara ya Afya .
Naye
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Ufuatiliaji wa Magonjwa na Epidemiolojia
Wizara ya Afya Dkt.Vida Mbaga amesema mazoezi husaidia kupunguza uzito na
kudhibiti kiwango cha sukari mwilini huku Asteria Shirima kutoka sehemu ya
Elimu ya Afya kwa Umma akisema elimu ya afya ikiwemo lishe bora na umuhimu wa
mazoezi imekuwa ikitolewa kwa jamii inayohudhuria katika mazoezi hayo.
Ikumbukwe
kuwa Idara ya Kinga, Wizara ya Afya imeanzisha Mpango kwa watumishi
kufanya mazoezi mara mbili kwa wiki Jumatano na Ijumaa jioni mara baada ya saa
za kazi kuanzia saa 9:30 hadi saa 11:00 jioni hiyo ni katika kuungana na
mkakati endelevu wa Wizara ya Afya wa Kupambana na Magonjwa Yasiyoambukiza.
Post a Comment