Kikosi Maalum cha Wanamgambo nchini Sudan cha
RSF, kimesema kimechukua udhibiti kamili wa Ikulu ya rais, makaazi ya mkuu wa
jeshi Jenerali ABDEL FATTAH AL-BURHAN na uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Khartoum.
Katika taarifa yake iliyotolewa Jumamosi, RSF imesema imechukua pia udhibiti wa viwanja vingine viwili vya ndege, kwenye mji wa kaskazini wa Merowe na mji wa El-Obeid ulioko upande wa kusini mwa nchi.
Tarifa hiyo imeeleza kuwa hatua hiyo
imechukuliwa katika kujibu mashambulizi yanayofanywa na jeshi dhidi ya kambi za
RSF kusini mwa mji mkuu, Khartoum.
Awali kikosi cha RSF kinachoongozwa na
Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo, anayefahamika zaidi kwa jina la Hemedti,
kilisema kuwa jeshi lilizingira moja ya kambi zake na kufyatua risasi kwa
kutumia silaha za kivita.
Wakati huo huo, vyama vya kiraia vya Sudan
ambavyo vimesaini makubaliano ya awali ya kugawana madaraka na jeshi la nchi
hiyo pamoja na kikosi cha RSF vimetoa wito wa kusitishwa kwa mapigano
yaliyozuka baina ya vikosi hivyo viwili.
Kwa mujibu wa vyama hivyo pia vimetoa wito
kwa wadau wa kimataifa na kikanda kuchukua hatua haraka kuzuia umwagaji damu.
Credit: DW
Post a Comment