YOUR FUTURE IS CREATED BY WHAT YOU DO TODAY, NEVER TOMORROW

Mchunguzi wa masuala ya Haki za Binadamu wa Peru ametangaza kifo cha mtu mmoja katika mji wa Arequipa na kuongezeka kwa vifo vya watu wawili kutokana na ghasia ya siku ya Jumatano hatua iliofikisha jumla ya vifo 45, nchini kote kufuatia maandamano yanayoshinikiza rais wa taifa hilo la Amerika ya kusini ajiuzulu na kuitishwa kwa uchaguzi mwaka huu 2023.

Rais wa Peru Dina Boluarte

Na Mwandishi wetu

Katika mji wa kusini wa Arequipa, waandamanaji takriban 1,000 walijaribu kuvamia uwanja wa ndege siku ya Alhamis, lakini walizuiliwa na polisi waliofyatua mabomu ya machozi. Waandamanaji hao ambao wamesambaa katika mji mkuu wakitokea kwenye mikoa mbalimbali walilenga kufika kwenye ikulu yenye ulinzi mkaali hapo jana Alhamis.

Mmoja wa waandamanaji amekaririwa na vyombo vya habari akisema maandamano hayo yanalenga kupigania haki yao ya kidemokrasia.

Rais wa Peru Dina Boluarte Katika hotuba yake iliofuatiliwa kwa ukaribu na waandamanaji wakitaka kujua kama wamejibu hoja zao amesema hakuna faida katika maandamano hayo yaliyosababisha machafuko na kuyataja ni kinyume cha sheria. "Mnadai madai nje ya utawala wa sheria mkitaka kuiondoa serikali." Amesema Bi. Boluarte

Bi Boluarte, mwanasheria mwenye umri wa miaka 60, ni C, ikiwa tangu ipate uhuru wake zaidi ya miaka 200 iliyopita. Pia amesema anaunga mkono uchaguzi wa Rais na wabunge kufanyika 2024 ikiwa hapo awali ulipangwa 2026.







Post a Comment

Previous Post Next Post