YOUR FUTURE IS CREATED BY WHAT YOU DO TODAY, NEVER TOMORROW



Kwa wale waongea KISWAHILI na kiingereza cha darasani, nani kati yenu anataka nifanye ujinga ndipo mnisaidie?
Ni kiasi gani tunasisitizana kuwa na Upendo na kuwa na moyo wa kusaidiana hata kugawana tulichonacho. Japokuwa si kila wakati nitakupa sawa na nitakachobaki nacho mimi. Lakini si haya machache…! 

Ajabu leo mtu anagawiwa maarifa eti kwa sababu anahisi kuna manufaa kwa mgawaji tena hata asijue hakika yake, akapuuza alichostahili. Nani ana nafasi mbili za mafanikio na ana hakika hata leo siyo masikini na aliyekosa mafaniko aliyoyataka? Tusilishane ujinga na tukashangilia huku tukiendelea kuwatazama macho meupe wanaotuzubaisha.

Nikiwa mtanzania ndani ya nchi yangu ambayo wakazi wake walichagua lugha ya Kiswahili kutumika kama lugha ya taifa katika mawasiliano na baadaye Kiingereza kama lugha ya ofisini, hii yote ni mali yangu. LUGHA.

Watoto tangu wanapokuwa wamefikia umri wa kuenda shule, mwalimu wake wa elimu ya awali anamfundisha kutamka maneno mageni, na yale ya lugha zinginezo yakiwemo. Kiingereza hata lugha za kibantu wakati wa kueleweshana kati ya mwalimu na mwanafunzi haswa katika shule zipatikanazo maeneo ya vijijini. Ahsante watanzania wote tunajua kusoma na kuandika na kama huwezi vyote basi unaweza kutazama picha na ukaelewa.

Lakini,tusitumie uelewa wetu kama silaha za kuangamizana wenyewe, maana ndivyo ilivyotakiwa kuwa toka katika dhamira ya aliyetuaminisha hivyo. Bali tuone njia ya kuutafuta muafaka na kutatua haya machache ambayo yanatokana na uchochezi wa haya mataifa MOTO MOTO, nayaita hivyo. Tumia uelewa kujua lengo lao ni lipi na tunawezaje kutengeneza udhaifu katika ngwe hii shuruti kwa vizazi vyetu tulivyonavyo na vijavyo hofu juu ya Vitakavokuwa vyao.

Lingekuwa jambo jepesi ningeandika mashairi kadhaa ukawa mziki. Nimehitaji chombo cha habari, nacho kinanipatia changamoto tofauti. Iko hivi …… Itaendelea

USIKOSE KUFUATILIA MACHAPISHO YA KILA SIKU ILI UPATE KUFAHAMU NJIA MBALIMBALI ZA ULAGHAI MJINI HASA KATIKA TASNIA MAMA KWA VIJANA WETU TANZANIA. 
Tembelea kurasa zetu katika mitandao ya kijamii:
facebook | instagram
@muzikihuru

Post a Comment

Previous Post Next Post