Mbunge wa Mtama na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema video inayosambaa ikimuonesha akisema kuna mbinu nyingi za kushinda Uchaguzi ikiwamo zisizo halali imepotoshwa na hakuwa na maana kama iliyotafsiriwa na Watu wengi Mitandaoni.


Kupitia ukurasa wake katika Mtandao wa X, leo Julai 16, 2024 ameandika “Nimeona mjadala wa video hii; inapotoshwa kwa kukata vipande watakavyo wapotoshaji. Msingi wa mjadala huu ulikuwa utani wa hoja ya zamani ya “Goli la mkono” uliorushwa wakati naongea ndio maana kuna kicheko kabla.”

Ameongeza “Haikuwa ‘serious version’. Mimi muumini wa uchaguzi huru na haki. Vizuri tuendelee kushindana kwa hoja.”


Post a Comment

Previous Post Next Post