Serikali inaendelea na utekelezaji wa shughuli za usafi wa Mazingira na uboreshaji wa miundombinu ya matundu 100 ya vyoo katika shule zilizokuwa zikitumika kuhifadhi waathirika wa maporomoko ya udongo wilayani Hanang Mkoani Manyara. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa afua mbalimbali zenye lengo la kurudisha hali katika uhalisia wake. Uboreshaji wa vyoo katika Shule hizi unasaidia kuweka utayari wa mazingira safi pindi shule zitakapofunguliwa Mwezi Januari.
Mkuu
wa Sehemu ndogo ya Maji na Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Afya
Anyitike Mwakitalima akizungumza katika zoezi la ukarabati wa matundu 32
ya vyoo shule ya Msingi Gendabi amesema uwekaji wa matundu ya vyoo ya
kisasa utasaidia wanafunzi kufurahia Mazingira ya kujifunzia kutokana na
ubora wa vyoo hivi ambavyo hutumia maji kidogo na hudhibiti harufu
mbaya pamoja na wadudu .
“Vyoo
vilivyokuwepo vilikuwa na mapungufu kadhaa ambayo tumebaini hivyo,
tumeamua kuboresha ambapo kutakuwa na faida nyingi ikiwemo utumiaji wa
maji kidogo, hakutakuwa na harufu mbaya, wadudu kama mende hawatakuwepo
na hofu ya kutumbukia haipo hata mtoto anayetambaa hawezi kutumbukia
,pia wadudu hatarishi kama nyoka hata akitumbukia hataweza kutoka tena
maana kina mfuniko unaojifunika”amesema.
Aidha
, Mwakitalima amewahakikishia Wazazi kuwa baada ya kambi kufungwa
Mazingira ya shule ni salama kwani tayari wameshanyunyizia dawa kuondoa
wadudu na mazingira yanakuwa bora zaidi kuliko awali.
Naye
Muuguzi Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara Editha Jonathan
amesema usafi wa mazingira na ukarabati wa miundombinu ya vyoo utasaidia
kuepuka magonjwa ya mlipuko huku akisema usambazaji wa jumbe za
uelimishaji kuhusu masuala ya afya umekuwa ukiendelea.
Kwa
upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Shule ya Msingi Gendabi Mwalimu
Kindoli Twaha ameshukuru hatua hiyo ya uboreshaji wa miundombinu ya
matundu ya vyoo.
“Maboresho
haya tunayafurahia sisi kama walimu maana mwanafunzi hawezi kuona
tundu la choo na vinatumia maji kidogo sana”amesema.
Post a Comment