Anamringi
Macha ameteuliwa na vikao vya chama cha Mapinduzi kuwa Naibu Katibu Mkuu
Bara jana Novemba 29, 2023 akichukua nafasi ya Christian Mndeme.
Mwezi
July 2023 Anamringi aliteuliwa na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano
Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kuwa mkuu wa wilaya ya Kahama na
kuchukua nafasi ya Fadhili Nkurlu ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Itakumbukwa
January 20, 2020 akiwa mkuu wa wilaya, Anamringi Macha aling’ara katika
vichwa vya habari baada ya kuonekana akigawa ndizi na mahindi ya
kuchemsha kwa Wananchi waliopanga foleni kufuatilia namba za NIDA ili
waweze kusajili laini zao kwa alama za vidole na kuepuka kufungiwa
kutokana na tangazo lililotolewa na TCRA.
Macha amewahi kuwa mkuu
wa mkoa wa Shinyanga, katibu msaidizi wa CCM kuanzia ngazi za wilaya na
baadaye akashikilia nafasi hiyo katika ngazi ya mkoa. Aidha amewahi
kuwa katibu msaidizi mkuu idara ya uenezi na katibu wa sekretarieti.
Post a Comment