YOUR FUTURE IS CREATED BY WHAT YOU DO TODAY, NEVER TOMORROW

Pele, gwiji wa soka na mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil aliyekulia kwenye umaskini na hatimaye kuwa mmoja wa wanamichezo wakubwa duniani, amefariki jana Alhamisi akiwa na umri wa miaka 82.

Taarifa ya Hospitali ya Albert Einstein iliyoko mjini Sao Paulo, ambako Pele alikuwa akipokea matibabu, imesema gwiji huyo wa kandanda alifariki saa tisa na dakika 27 alasiri kutokana na viungo vyake kushindwa kufanya kazi.

Pele alikuwa akiugua saratani ya utumbo.

Kifo cha Pele, ambaye ni mchezaji pekee aliyeshinda Kombe la Dunia la FIFA mara tatu mwaka 1958, 1962 na mwaka 1970, kilithibitishwa kupitia akaunti yake ya mtandao wa Instagram kwa taarifa iliyoandikwa;

"Msukumo na upendo ndio sifa zilizopamba safari ya Mfalme Pele, aliyefariki dunia leo," Na kuongeza "aliiletea dunia furaha kutokana na kipaji chake katika soka, alizuia vita, alifanya kazi za kijamii duniani kote na kueneza kile alichoamini kuwa tiba ya matatizo yetu yote: upendo."

Salamu za rambi rambi zinaendelea kumiminika kutoka kile pembe ya dunia- kutoka kwa watu maarufu katika fani ya michezo, siasa, burudani, sanaa na tamaduni, kwa mtu maarufu aliyeiweka Brazil katika ramani ya soka duniani.

Hakika atakumbukwa kwa alama ya ubora aliyoiacha katika ulimwengu wa soka.





Post a Comment

Previous Post Next Post