Jeshi
la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata simu 61 kutoka kwa wanawake watatu wanaofanya shughuli za wizi kwenye maeneo ya minada na hukwapua mali hizo wanapolala na
wanaume.
Akitoa
taarifa kwa vyombo vya habari Disemba 20, 2023 Kamanda wa
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amesema simu hizo na
watuhumiwa watatu wamekamatwa katika misako inayofanywa na
jeshi la polisi kwa lengo la kuimarisha Usalama wa Raia na Mali zao hasa
katika kipindi hiki kuelekea Sikukuu za Chrismas na Mwaka mpya ili
kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Shinyanga wanasherekea Sikukuu hizo kwa
amani na utulivu.
"Tunawashikilia
wanawake watatu raia wa Burundi ambao wameingia nchini kwa njia haramu
na wamekuwa wakifanya wizi, tumewakamata wakiwa na simu 61 walizoiba
kwenye minada ya Kahama, Mwanza na Shinyanga. Lakini akina dada hawa
pindi wanapolala na wanaume huwaibia na kuwatoroka wanaume hao",amesema Kamanda Magomi.
"Kufuatia
Doria na misako hiyo iliyofanyika katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa
Shinyanga, Mwezi Novemba 30, 2023 hadi Disemba 19, 2023 Jeshi la Polisi
Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata Simu 61 ambazo zimekamatwa
kutoka wa akina dada waliokuwa wanafanya shughuli za wizi, pombe ya
moshi Lita 173, mafuta ya dizeli Lita 260, Pikipiki 07, TV 04, vyuma vya
kuchimbia visima 09, Goroli za Karasha 106, Bangi misokoto 15,
Subwoofer 02, Difu 01 ya Gari aina ya Toyota Hiace pamoja na noti bandia
09 zenye thamani ya Tshs.85,000/=",ameeleza Kamanda Magomi.
Amevitaja
vitu vingine vilivyokamatwa ni pamoja na Pipe 11 za kunyonya mafuta,
Baiskeli 01, vipande vya nondo 06, Keyboard 01, Chesess 01 ya Pikipiki,
Spika 02, na vifaa mbalimbali vya kupigia ramli chonganishi ambavyo ni
mikia 08 idhaniwayo kuwa ni ya mnyama aina ya Nyumbu, kipande 01 cha
Ngozi ya Simba.
Katika
upande wa mafanikio ya kesi Mahakamani, Kamanda Magomi amesema jumla ya
kesi 08 zilipata mafanikio ambapo kesi 01 ya kubaka mshitakiwa
alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, kesi 02 za kujipatia pesa kwa
njia ya udanganyifu washitakiwa walihukumiwa kwenda jela kati ya miezi
06 hadi miaka 03.
"Nyingine
ni kesi 01 ya kuharibu mali mshitakiwa alihukumiwa kwenda jela miezi
05, kesi 02 za wizi wa pikipiki washitakiwa walihukumiwa kwenda jela
kati ya miaka 02 hadi 03, kesi 01 ya kupatikana na mali idhaniwayo kuwa
ya wizi mshitakiwa alihukumiwa kwenda jela mwaka 01, Kesi 01 ya wizi wa
kuaminiwa washitakiwa 06 walihukumiwa kutotenda kosa lolote kwa mwaka
01. Kesi 01 ya kutishia kuua kwa Silaha panga mshitakiwa alihukumiwa
kutotenda kosa lolote kwa mwaka 01",ameongeza.
Aidha
katika kudhibiti ajali za Usalama Barabarani Jeshi la Polisi Mkoa wa
Shinyanga limefanikiwa kukamata jumla ya makosa mbalimbali 2806, kati ya
hayo makosa 05 yalikamatwa kwa kusababisha ajali, kuendesha mwendokasi
na matumizi mabaya ya barabara na madereva kulipa faini.
"Pamoja
na hatua mbalikmbali tunazoendelea kuzichukua katika kudhibiti ajali za
barabarani pia Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga
kimefanikiwa kutoa elimu kwa makundi yote yanayotumia barabara kwa lengo
la kupunguza ajali za barabarani na linawasisitiza madereva kufuata
sheria wenyewe bila kusimamiwa na askari, dereva yeyote atakayevunja
sheria atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria",amesema.
Post a Comment